CUF YATOA MSIMAMO JUU YA SIKU YA HABARI DUNIANI
The Civic United Front-CUF Kinaungana na waandishi wote wa
habari nchini katika kuadhimisha siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani. CUF – Chama cha Wananchi kinatambua
kwa dhati mchango muhimu na mkubwa wa waandishi wa habari katika kustawisha na
kuimarisha demokrasia nchini.
Katika kuadhimisha
siku hii adhimu, CUF - Chama cha Wananchi kinaendelea kuwaomba waandishi wote
wa habari wa ndani na nje ya nchi kufanya kazi na kutekeleza wajibu wao kwa kuzingatia maadili ya taaluma
ya habari bila ya khofu, woga na wasiwasi wa aina yoyote unaopandikizwa kwao
kwa lengo la kunyamazisha sauti zao na vyombo wanavyo viwakilisha.
Aidha CUF-Chama
cha Wananchi, kinatambua wazi kwamba, Tasnia nzima ya habari pamoja na
waandishi wa habari Tanzania, wameendelea kufanya kazi katika mazingira magumu,
yasio huru na yalio jaa vitisho na vikwazo dhidi ya kazi zao.
Kwamba,
maendeleo ya tasnia ya habari yameendelea kudidimia, kutokana na ongezeko kubwa la vitisho dhidi ya
waandishi wa habari, kama kupotea, kutekwa na kupigwa hadharani kwa baadhi ya
waandishi wa habari pamoja na mabadiliko ya kikanuni yanayo minya uhuru wa
kutanuka kwa uhuru na upatikanaji wa habari.
CUF-Chama cha
Wananchi kinatoa rai kwa wadau wa habari na Tasnia nzima kwa ujumla kuendelea
kupigania uhuru wa habari kwa nguvu zote, kwasababu anguko la Tasnia ya habari
ni anguko la Demokrasia na Taifa kwa ujumla.
CUF-Chama cha
Wananchi kiko bega kwa bega katika kuhakikisha uhuru wa habari Tanzania
unaendelea kulindwa na kuheshimiwa pamoja na kuendelea kufanya kazi kwa karibu
sana na waandishi wa habari kwa maslai ya Taifa.
Imetolewa leo, Tarehe 03.05.2018 Na.
MH. SALIM BIMANI
MKURUGENZI WA HABARI, UENEZI NA MAHUSIANO YA UMMA
Hakuna maoni