Recent Posts

Breaking News

Muungano wa zanzibar na Tanganyika bado ni kaa la moto


TAMKO RASMI April 11, 2018. Jumuiya Ya  Wazanzibari Waishio Nchini Marekani (ZADIA), inapenda kuungana na Wazanzibari  wote,  ndani na  nje  ya  Zanzibar,  katika  kuunga  mkono msimamao  madhubuti wa kizalendo uliodhihirishwa na  Wabunge kutoka Zanzibar katika Bunge la Jamhuri  ya Muungano  wa Tanzania.

 Itakumbukwa kuwa  mnamo  siku  ya  Jumatatu  tarehe  09  April,  2018,  Wabunge kutoka Zanzibar,  bila kujali itikadi zao  za kisiasa,  walitoka nje  ya  Bunge  wakati wa  kikao cha Bajeti  ya Waziri Mkuu wakilalamikia kudhalilishwa kwa hadhi  ya Zanzibar ndani  ya Muungano  na ndani  ya  Bunge hilo.

ZADIA  inaamini kuwa Tanzania ni Muungano wa nchi  mbili  zenye  hadhi  sawa, (Tanganyika na Zanzibar)  zilizoungana na kuunda  kilichojulikana kama  Jamhuri  ya Muungano  wa  Tanganyika na  Zanzibar na  baadae Jamhuri  ya  Muungano wa  Tanzania, na kwamba  Serikali  ya  Tanzania haina  mamlaka juu  ya  Serikali  ya Zanzibar  yenye  Taasisi zake kamili na imara.  Kwa  hivyo inaunga  mkono kauli  ya  Wabunge hao  Wazalendo waliyoitoa  wakiongozwa  na  Mheshimiwa  Ally  Saleh  (Mbunge  –  CUF  Malindi,  Zanzibar) kupinga  vitendo  na  kauli  za  kuidhalilisha  Zanzibar  ndani  ya  Bunge  na  katika  Serikali  ya Tanzania. Aidha, ZADIA inapenda kutoa pongezi rasmi  kwa Mheshimiwa Sada Mkuya (Mbunge  – CCM  Welezo,  Zanzibar) kwa  ujasiri wake  wa kusimama  kidete  na kutetea hadhi na maslahi  ya Zanzibar ndani  ya Bunge la Jamhuri  ya  Muungano wa  Tanzania. Tunapenda kumthibitishia  kuwa  Wazanzibari  wote,  bila  kujali  tofauti  zao  za  kisiasa,  kijinsia  na nyenginezo  wako pamoja  naye  katika  mapambano  ya  kupigania haki  na  hadhi  ya Zanzibar tuipendayo  ndani  ya Muungano  wa  Tanzania  na duniani kote.

Hakuna maoni