Recent Posts

Breaking News

Arsenal walilaza Stoke 3-0.

Arsene Wenger anaamini kwamba hali ya klabu hiyo kutofana katika Ligi ya Premia ndiyo iliyochangia mashabiki wa klabu hiyo kutojitokeza kwa wingi wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya England dhidi ya Stoke Jumapili.


Gunners walizomewa na mashabiki wakati wa mapumziko uwanjani Emirates, baada ya Aaron Ramsey kugonga mwamba wa goli kwa kombora lake ambayo ilikuwa nafasi pekee kwa Arsenal kupata dakika 45 za kwanza.
Lakini Pierre-Emerick Aubameyang alifunga penalti iliyopatikana kwa njia ya utata, baada Bruno Martins Indi kumchezea visivyo Mesut Ozil, na kuwazawadi bao la kwanza kipindi cha pili.
Mshambuliaji huyo wa Gabon aliongeza la pili kupitia kona iliyopigwa na Ozil.
Aubameyang kisha alikosa kutumia nafasi ambayo ingemuwezesha kupata hat-trick walipopata penalti nyingine baada ya Badou Ndiaye kumsukuma na kumwangusha Alexandre Lacazette.
Alimwachia Lacazette apige mkwaju huo na akafunga
Arsenal, ambao watakuwa wenyeji wa CSKA Moscow katika ligi ndogo ya klabu Ulaya Europa League Alhamisi, wamesalia alama 13 nje ya eneo la kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya Tottenham kulaza Chelsea 3-1 Jumapili.
Wenger anasema anafahamu ni kwa nini hakukuwa na mashabiki wengi uwanjani Emirates.

Hakuna maoni