Recent Posts

Breaking News

BAVICHA YATEMA CHECHE.



BARAZA la Vijana la  Chadema (Bavicha) limejiapiza kukulinda chama chao kwa gharama yeyote kwa kile walichodai ni hujuma za kutaka kukifuta na kufungwa kwa viongozi wa chama hicho. 
wenyekiti wa Bavicha, Patrick Ole Sosopi amesema kuwa vijana wa Chadema ndiyo walinzi wa chama hicho ambapo ameahidi kupitia vijana hao chama kitalindwa dhidi ya hujuma.
Amesema kuwa chama hicho kipo kwenye hujuma zilizopangwa makusudi ili chama tawala ambacho ndicho chama dola ambacho kimetani kibaki chama kimoja.
Ole Sosopi amesema kuwa kushikiliwa kwa viongozi wa juu wa chama hicho ni sehemu ya mkakati huo ambapo ameeleza jinsi viongozi hao walivyokamatwa na kufikishwa mahakamani kimya kimya ikiwa muda umeenda hadi kukosa dhamani kuwa ni mkakati wa kuwafunga.
Amesema kuwa hujuma hizo zimemuibua msajili wa vyama vya siasa ambaye amekuwa akitumia mwamvuli huo kutaka kukihujuma chama kwa kutishia kukifuta.
Amemtaja Cyprian Musiba ambaye amekuwa akiwatukana na kukashifu viongozi wa chama hicho bila kuchukuliwa hatua yoyote kisheria ilhali anavunja sheria ambapo anaonekana kuwa sehemu ya mkakati huo.
Mwenyekiti huyo amesema kuwa hawatarudi nyuma kwenye uamuzi watakao uwelekeza kwa wafuasi vijana wa chama hicho.
“Bavicha iliyopo chini yangu sio ile ya Katambi (Patrobas) lakini hata kipindi kile mimi ndiye niliyekuwa nikihamasisha hatua kadhaa kwenye chama. Bavicha hii haitarudi nyuma,” amesema Ole Sosopi.
Wakati huohuo, Ole Sosopi amesema viongozi na wafuasi wa chama hicho wataenda mahabusu kuwafariji na kusherehekea pamoja Sikukuu ya Pasaka kwenye gereza la Segerea jijini Dar es Salaam na gereza la Ruanda Mbeya alikofungwa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’.

Hakuna maoni